Saturday 3 March 2012

IMANI POTOFU KUHUSU AFYA YA KINYWA NA MENO


Na Dr. Augustine Mbehoma Rukoma
Asante kwa mtandao kwani habari zinasambaa haraka kama mwanga. Hata hivyo, uvumi, imani potofu vinasambaa kwa kasi ile ile pia. Hii inahusisha imani potofu kuhusu afya ya kinywa na meno. Kwa hiyo,
nafikiri ni bora kuchukua muda kidogo kuweka baadhi mambo sawa kuhusu afya ya kinywa na meno.
Baadhi ya imani potofu ni kama ifuatavyo:-

1.      POTOFU: Kupiga mswaki mara nyingi na kwa nguvu huzuia kuoza kwa meno
UKWELI: Si mara ngapi unapiga mswaki na nguvu gani inatumika, suala ni unapigaje mswaki. Kupiga mswaki mara nyingi na kwa maguvu kunaweza kupleleke kukwangua sehemu ngumu ya nje ya jino, kulifanya laini na hatimaye kuuma au hata kuvunjika. Kupiga mswaki mara mbili, taratibu na kwa njia sahii ndicho kinachosaidia meno kuwa na afya

2.      POTOFU: Huna haja ya kumuona tabibu wa meno kama hujaona au kuhisi una tatizo la meno.
UKWELI: kila mtu anatakiwa kumuona tabibu wa meno angalau mara mbili kwa mwaka bila kujari meno yake yanaonekana vizuri au imara kiasi gani. Si meno yote yanayoonekana mazuri na imara ni mazima, mengine yanaweza kuwa yameoza katika maeneo usiyoweza ona kama chini ya fizi na kwenye mizizi, si hivyo tu hata uoto mpya (neoplasm) uweza kugundulika mapema kabla ya kufanya uaribifu mkubwa kama utachunguzwa na wataalamu. Kumbuka pia mangonjwa ya mifumo mingine kama ukimwi,
kisukari na mengine mengi hujidhihilisha mapema kinywani kabla mgonjwa hajapata dalili zingine.

3.      POTIFU: Husile kitu chochote unapokwenda kung’oa jino
UKWELI: Njaa inaweza kukufanya uzirahi katika zoezi la kungoa jino, hofu ikichanganyika na sukari kidogo mwilini husababisha ubongo kushindwa kufanya kazi sawa sawa. Imani hii potofu inahusishwa na
sindano ya ganzi, watu wengi wanafikiri kila ganzi inatakiwa mtu awe hakula kwa muda Fulani. Hii kwa matibabu ya meno sio kweli kwani ganzi utolewa kwenye eneo husika tu (local anaesthesia) hivyo haiathili mwili mzima.

4.      POTOFU: Husitoe jino au kufanya matibabu ya mzizi wa jino kama una uvimbe hasa usaa
UKWELI: Kung’oa jino au matibabu ya mzizi wa jino yanasaidia kutoa nafasi/njia kwa usaa kutoka na hivyo kupona haraka pengine bila hata kuhitaji dawa (antibiotics). Yaweza kuwa kweli pale tu kama mgonjwa atukuwa na homa au hawezi fungua kinywa ambapo itabidi udhibiti homa kwanza, na kama ni
kushindwa kufungua kinywa yabidi kuacha na kutibu kinacho mfanya ashindwe kufungua kinywa kwanza.

5.      POTOFU: Mama mjamzito hastahiri kutoa jino mpaka atakapo jifungua
UKWELI: Kumuacha mama mjamzito na maumivu pamoja na ugonjwa kwaweza kufanya ugonjwa kusambaa na kuingia kwenye ubongo hata kupelekea kifo cha mama na mimba yake. Pia maumivu makali yaweza kusababisha mimba kutoka.

6.      POTOFU: Njia ya uhakika ya kutibu jino ni kuling’oa
UKWELI: Ziko njia nyingi na za uhakika za kutibu jino bila kungoa. Kung’oa jino kama tiba ni pale tu ambapo jino hilo haliwezi tibika kwa njia yeyote na kukaa kwake kwa weza leta madhara zaidi. Kutoa jino huleta madhara mengine na meno bandia pamoja na kwamba hayawezi kurejesha kazi za meno yaliyotoka kwa kiwango halisi, lakini pia utunzaji wake ni mgumu na gharama pia. Hata hivyo kama umelazimika kupoteza meno basi meno bandia ndilo chaguo pekee.

7.      POTOFU: Kuweka dawa ya kutuliza maumivu kama aspirini kwenye tobo kunasaidia kutoa maumivu.
UKWELI: Kama ilivyo kwa magonjwa mengine, kutuliza maumivu wakati kisababishi cha maumivu hakijashugulikiwa ni kulikuza tatizo kwa gharama. Mbali na hivyo dawa kama aspirini uunguza fizi zilizozunguka jino ulimoiweka, pia ulilainisha? (weaken) na kufanya uotaji wake uwe
mgumu kwani uvunjika vunjika ovyo ovyo

8.      POTOFU: Kutoa jino husababisha kifo
UKWELI: kuendelea kukaa na jino lililooza na halifai kuzibwa hufanya ugonjwa kusambaa na kusababisha kifo. Unaonekana kama ukweli pale tu mgonjwa anakuja hospitalini kutoa jino
9.      POTOFU: Meno mazuri urithishwa (inherited)
UKWELI: Eti kwa vile tu mama au baba ana meno mazuri na mazima na wewe utakuwa hivyo au kinyume chake. Uridhi unachangia kiasi kidogo sana, utunzaji wa meno vizuri na kukutana na tabibu wa meno mara kwara ndio mambo muhimu ya kuweka meno na kinywa chako sawa.

10.     POTOFU: Hakuna haja ya kuangaika na meno ya utotoni kwani yatatoka baada ya muda wake kufika
UKWELI: meno ya utotoni yasipotunzwa vizuri yanaweza kusababisha kutoka/ kutolewa kabla ya muda wake na kupeleke meno ya ukubwani kuota kwa mpangilio usiopendeza, lakini pia katika kipindi cha mchanganyiko wa meno ya ukubwani na utotoni, meno ya utotoni yaliyooza yaweza ambukiza ya ukubwani.

11.     POTOFU: Maumivu ya meno yatajiishia yenyewe baada ya muda.
UKWELI: Kama jino limeoza haliwezi pona kwa namna yoyote mpaka lipate tiba hata kama haliumi. Ukiendelea kulidharau ugonjwa uweza kusambaa mpaka maeneo mengine kama ubongo, kifuani na hatimaye kusababisha kifo.
Angalizo: Ni asilimia tano tu kati ya wagonjwa ambao tatizo la jino
limesambaa hadi kwenye ubongo uweza kupona.

Tafakari chukua hatua 2012

Saturday 10 December 2011

MATIBABU YA MZIZI WA JINO (ROOT CANAL TREATMENT)

Na Dr. Augustine Mbehoma Rukoma (DDS, MDent-restorative Dentistry)
Haya ni matiba ambayo hutolewa kwa jino ambalo sehemu ya uhai wake imearibika kiasi kwamba aliwezi kutibika kwa kuziba tu, kwa maneno mengine hii ndio njia mbadala ya kutibu jino bila kung’oa.
Matibabu huusisha kutoboa jino hadi sehemu ya uhai wa jino yenye mishipa ya damu na iliya ya fahamu na chembechembe za meno na kuviondoa nikimaanisha kuondoa mishipa ya fahamu, ya damu na chembe pamoja na ugonjwa na baadae kuijaza sehemu hii na vitu mahalumu vinavyokubaliana na mwili (biocompatible).
Aina za matibabu ya mziizi wa jino
Kuna aina kuu mbili za matibabu ya mzizi wa jino
1.      Nia ya kawaida (conventional root canal treatment)
Njia hii ni kama nilivyoeleza hapo juu, kuingia kwenye kiini cha jino na kuondoa kila kila kilichomo na kasha kujaza uwazi na vitu maalumu vinavyokubaliana na mwili
2.      Matibabu ya mzizi wa jino yanayohusisha upasuaji,
kwa njia hii mbali na kutumia njia ya kwanza, upasuaji hufanyika pia ili kondoa mfupa uliofunika ncha ya mzizi wa jino kusafisha eneo lililozunguka ncha ya mzii na baadae kukata ncha husika kasha kuziba kutokea kwa nyuma (retro grade filling). Njia hii hutumika pale njia ya kawaida inaposhindwa kuondoa tatitizo au inapoonekana kabisa kuwa haitaweza kuondoa tatizo. Huu ni upasuaji mdogo, unaofanyika kwa ganzi ndogo ya eneo husika (local anaesthesia). Mafanikio ya matibabu haya ni makubwa sana
Ni meno yapi yanahitaji matibu hayo
·         Meno yaliyooza hadi uoza kufikia kiini cha jino (dental pulp)-sehemu ya uhai wa jino.
·         Meno yaliyopata ajari na kupasuka na kuacha kiini cha jino kikiwa wazi (traumatic pulp exposure)
·         Meno yaliyopata ajari na kusababibisha mishipa ya damu kukatika au kubasuka na kuvujia ndani ya jino, kitu ambacho hupelekea jino kufa (pulp necrosis) na baadae kusabisha jibu au kubadilika rangi
·         Wahati mwingi japo ni mara chache, ni pale tunakuwa tunata kuliweka sawa jino/meno ambalo/ambayo hayakoo kwenye mstari sawa ili yaendane na menzake
·         Pia wakati mwingine, tunapo lisaga jino ili liweze kubeba meno bandia ya daraja (bridge) huku tukiwa na mashaka na uahi wake.
Nini dalili zinazo ashilia jino kuhitaji matibabu haya
·         Jino linalo uma- kuuma kwa jino kunashiria ugonjwa kuwa umeingia ndani ya kiini cha jino na au hata kupitiliza na kuingia kwenye mfupa ulioshikilia jino
·         Jino lililo oza na kusababisha uvimbe, liwe linauma au haliumi
·         Jino lililokatika na kupoteza zaidi ya nusu ya kichwa cha jino (crown) kukatika kuwe kwa hajari au kuoza au vyote kwa pamoja
·         Jino linalobadilika rangi huku kukiwa na historia ya kuligonga mahali au kuchapwa ngumi usoni, hapa jino linaweza kuanza kubadilika rangi miezi sita tangu siku ya ajari mpaka wakati mwingine hadi miaka ishiri wakati mgonjwa aliisha sahau hata hajari yenyewe
Meno yasiyo faa kwa matibabu haya
·         Meno yaliyoaribika vibaya kiasi kwamba hayatibiki tena japo ni machache, kwani hata kama jino limebaki mzizi tu, ukiwa bado imara twaweza fanya matibabu haya na baadae kujenga kichwa (crown)
·         Meno yaliyolegea sana kutokana na magonjwa ya fizi ambayo hayawezi kuimalishwa tena
·         Magego ya mwishi (wisdom teeth) kwa kawaida meno haya huwa yana maumbile yasiyotabirika kiasi kwamba hata mafaninio ya matibabu hayatabiriki, hii ikiambatana na kuwa yako nyuma sana kiasi cha kuwa vigumu kuyafikia kwa ufasaha na vifaa vyetu na pia yana mchango kidogo kwa usagaji chakula (2%)
·         Meno ambayo mifereji ya mizizi ambayo hupitisha mishipa ya fahamu na damu imeziba (calcified root canals)
Mafanikio ya matibabu haya
Kiwango cha mafanikio ya matibabu haya ni kati ya asilimia sabini na saba hadi tisini na nane (77-98%)
Haya ni mafannikio ya hali ya juu kwa matibabu ya aina yeyote ile, mafanikio uongezeka zaidi pale tabibu anapotumia vifaa vya kumuongezea uwezo wa kuona kama dental loops na operating microscope.
Kutokufanikiwa kwa matibabu haya
Ziko sababu mbali mbali zinazoweza kusababisha matibabu haya yasifanikiwe, baadhi zikitokana na udhaifu wa tabibu na zingine kutokana na jino lenyewe lilivyo (internal tooth morphology)
Tabibu-tabibu kama hakusafisha jino vizuri na kuliziba sawasawa upo uwezekano mkubwa wa matibabu haya kutokufanikiwa, pia tabibu kama hajui maumbili ya ndani ya jino vizuri, kuna uwezekana sehemi zingine kuachwa bila kusafishwa.
Meno –meno mengine yana maumbile yasiyo ya kawaida, mfano katika hali ya kawaida meno ya mbele yana mfereji mmoja wa kupitisha mishipa ya fahamu na damu, lakini kuna jino linguine linakuwa na miwili au mitatu, hapa kwa mazoea na kwa kukosa vifaa vya kisasa ni rahisi kusafisha mfereji mmoja na kuacha mingine, vivyo hivyo kwa magego ambayo kwa kawaida yana mifereji mitatu hadi mine, lakini mengine mitano, sita, saba hata utafiti Fulani huko china umegundua badhhi ya magego kuwa na matundu nane, meno ya namna hii ni vigumu kufanikiwa.
Nini kifanyike ili kupunguza uwezekano wa matibabu kutokufanikiwa?
Tabibu lazima ajikumbushe maumbile ya ndani ya jino analotaka kulitibu kabla ya kuanza matibabu na pia ajue kwamba jino laweza kuwa na mifereji ya ziada hivyo ajitahidi kuitafuta.
Matumizi ya vifaa vya kusaidia kuona ni muhimu na hata matumi ya x-ray za kisasa kama 3 dimensional digital x-ray ili kuweza kuona pande tatu za jino
Kwanini meno yanendelea kutolewa wakati matibabu haya yapo?
·         Matibabu haya ni gharama ukilinagisha na kung’oa jino hii ikienda pamoja na umaskini wa wananchi walio wengi, wanashindwa kuyagharamia na hivyo kuchagua kung’oa
·         Baadhi ya hospitali hazina wataalamu au vifaa vya matibabu haya au vyote kwa pamoja
·         Mwamko mdogo wa wananchi kuhusu matibabu ya meno, hii inachangiwa pia na tabibu wa meno kutokuelezea matibabu mbadala zaidi ya kung’oa, tafiti zimeonyesha baathi tabibu wa meno hutoa maelezo kwa yale matibabu wanayoyaweza tu, badala ya kuwaeleza pia upatikanaji wa matibabu mbadala katika sehemu zingine
·         Watu kuchelewa kufika hospitalini, wakija baadhi yao matibabu pekee yanayo kuwa yamebaki ni kung’oa tu, hapa napo kuna mchango wa umaskini na uelewa mdogo
·         Imani potofu kuwa tiba ya kudumu ya jino ni kuling’oa
·         Uzoefu wa zamani, kwa mtu ambaye aliwahi kuziba jino na likauma tena, ukimwambia matibabu haya ni vigumu kuyakubali
Hitimisho
·         Jali meno yako kama unavyojali viungo vingine vya mwili wako
·         Kungoa jino kama tiba ya ugonjwa wa jino, ni pale tu ambapo jino hilo haliwezi tibika kwa njia mbadala kama hii ya mzizi wa jino au pale inapobainika kuwa jino husika kuendelea kubaki pale hata likiwa limetibika linaweza kuwa chanzo cha kuleta madhara makubwa mwilini kama uoto mpya n.k.

Tuesday 8 November 2011

Watu wengine wanaweza kuwa na wenza wenye ukimwi bila kuambikizwa kwa muda mrefu au hata wasiambukizwe kabisa-taarifa (case report)

Na Dr. Augustine Mehoma Rukoma
Utangulizi
Neno ukimwi ni kifupisho cha maneno “Upungufu wa Kinga Mwilini”. Ugonjwa huu usabishwa na virusi ambavyo hushambulia chembe chembe za kinga na kuufanya mwili ushindwe kujilinda dhidi ya maradhi ipasavyo au hata kushindwa kupambana na maradhi yaliyoingia tayari.
Ukimwi uambukizwa kwa njia mbali kama; 1. kuingia damu ya mtu mwenye ukimwi kwa hasiye nao-hapo ndo kuna vitu kama kuchangia nyembe, sindano, kuwekewa damu isiyo salama n.k. 2. Kujamiiana- wadudu wa ukimwi wameonekana kuwemo kwenye majimaji ya sehemu za sili, hivyo kama kuna michubuko mtu akafanya tendo hili na mhadhilika kuna nafasi ya kuambukizwa. 3. Mama mjamzito kumuambukiza kiumbe kilichopo kwenye mfuko wakewa uzazi.
Japo si jukumu la makala hii lakini kinga ni pamoja na kuzuia kuchangia vifaa vyenye ncha kali, ktumia kinga unapofanya tendo la ndoa, kuacha kufanya tendo la ndoa kama unaweza na mengine.
Kwa vile kuna uwezekano wa kupata ukimwi kwa kutenda tendo la ndoa, wanandoa ambao kimsingi wengi wao kama si wote, hawatumii kinga wanapofanya tendo hili. Katika hali hii, kama kuna uwezekano mmoja ni muathilika, basi nafasi ya kumuambukiza mwenzake uongezeka.
Taarifa ya kwanza (case report 1)
Mwaka tisini na na sita, rafiki yangu mmoja, mtoto wake wa miezi mitatu alilazwa Muhimbili. Baada ya kuona maendeleo ya tiba si mazuri waliamua kumpima, majibu yakaonyesha ana virusi vya ukimwi. Majibu haya yalimfanya daktari aliyekuwa anamtibu mtoto kuwashauri wazazi nao wapime na wakakubli. Walipopima mama alikuwa mhathilika baba hapana, nawatu hawa walikuwa kwenye ndoa kwa muda wa miaka miwili, wakila tunda lao bila kinga.
Baada ya taarifa kufika kwa ndugu wa mwanaume wakashauri waachane wagawane walichochuma pamoja. Wakati wamepelekana mahakamani, mwanamke akana kwamba hawakuwahi kupima. Mahakama ikaamuru wapime, wakapima tena kwa hospitali chaguo la mwanamke. Majibu yakawa yale yale mama anao baba hana. Wakakubali kuachana na kugawana walivyochuma pamoja kama walivyoorodhesha mahakamani na baba kupangiwa kiwango cha kumlipa mama kwa malezi ya mtoto. Baada ya mwaka na nusu mtoto akapimwa tena na kugundulika hana ukimwi tofautu na alipokuwa amepimwa mwanzoni. Mpaka hapa ninapoandika wote wapo na afya njema, baba alioa mwanamke mwingine na wana watoto wawili na mama bado yupoanendelea kutumia dawa.
Uchunguzi usio rasmi ulionyesha mama alikuwa na ugonjwa huo hata kabla ya ndoa hiyo.
Taarifa ya pili
Jamaa yangu mmoja naye alikuwa ameoa na kualiwa watoto wanne katika ndoa yake. Ya miaka 15. Baadae  mwaka 2008 mke wake akaanza kuugua magonjwa ya ajabu ajabu, yanapona yanarudi na mapya yanajitokeza. Analazwa hospitali anaru tena baada ya muda, akaamua kwenda kwa mganga mpemba ambaye aliwambia mumewe ana mke mwingine kamtupia jini la damu. Akampa dawa hazikusaidia. Kutokana na lawama za hawala kuingia nabado hospitli na kwa waganga haponi, ikashauriwa wapime. Wakakubali. Walipopima mama anao baba hana. Mama akazidi kuamini kuwa hata kama ameonekana anaukimwi ametumiwa na huyo hawala wa mmewe. Ikawa kazi kumeza dawa, anaaza anaacha anakwenda kwa waganga wake, mara ya mwisho akaamua kuokoka sasa japo hapo kichwa nacho kilishaanza kuvurugika. Huko ndo kabisa akaambiwa aache dawa kabisa yesu atamponya. Mwanzoni mwa mwaka huu tumemzika.
Ninazo taarifa za namna hii nne lakini mbili zinatosha kutoa mjadala.
Mjadala
Katika taarifa zote mbili inaonyesha wahusika wote walishakaa pamoja wakila matunda yao bila kinga ndo maana wakapata watoto. Kwanini hawakuambukizana inawezekana walikuwa wanakula tunda lao bila michubuko yeyote katika kipindi chote walichokuwa pamoja. Sababu nyingine yawezekana wanaume hao wana kinga dhidi ya virusi vya ukimwi au chembe chembe zao za kinga hazina vipokezi (receptors) vya wadudu wa ukimwi. Tafiti zimeonyesha mdudu wa ukimwi huweza kuingia kwenye chembe chembe za kinga kupitia vipokezi katika hali ya kama ufunguo na kitasa au au nati na boriti. Kama mtu hana vipokezi hivi hawezi ambukizwa. Dr. Matthew Dolan, daktari bingwa katika jeshi la anga la marekani anasema, ansema Genetic resistance to AIDS works in different ways and appears in different ethnic groups. The most powerful form of resistance, caused by a genetic defect, is limited to people with European or Central Asian heritage. An estimated 1 percent of people descended from Northern Europeans are virtually immune to AIDS infection, with Swedes the most likely to be protected. One theory suggests that the mutation developed in Scandinavia and moved southward with Viking raiders.
All those with the highest level of HIV immunity share a pair of mutated genes -- one in each chromosome -- that prevent their immune cells from developing a "receptor" that lets the AIDS virus break in. If the so-called CCR5 receptor -- which scientists say is akin to a lock -- isn't there, the virus can't break into the cell and take it over. (haya yamenizengua kuyatafsiri)
Mtoto kuonekana ana ukimwi akiwa na miezi miatu na baada ya mwaka mmoja na nusu hana hii ni kutokana na ukweli kwamba mtoto anayezaliwa na mama mwenye virusi vya ukimwi huwa na antibodies dhidi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama yake. Unapopima ukimwi kutumia kipimo cha eliza ambacho uangalia antibodies hizi, basi mtoto huonekana hanao, lakini kama mtoto hakuambukizwa wadudu basi, antibodies hizi huondoka kwenye damu yake kadri muda unavyo kwenda.
Hitimisho
·         Kuna baadhi ya watu si rahisi kuwaambukiza ukimwi
Mapendekezo
  • Kutokupa  ukimwi kwa muda mrefu huku ukila tunda na mwenye nao kwa muda mrefu haikuhakikishii kuwa huwezi kuupata kwa hakikisha unafuata masharti ya kinga
  • Mtoto anayezaliwa na mama au wazazi wenye ukimwi si lazima awe nao fuata ushauri wa daktari na hasa kupima wakati wa ujauzito
  • Tuangalie namna ya kuwadhibiti waganga wa jadi na watumishi wa mungu wanashauri watu wasitumie dawa za kuongeza maisha

Thursday 20 October 2011

Yajue Baadhi ya Magonjwa Yenye Uhusiano Mkubwa na UKIMWI Katika Kinywa na Maeneo ya Uso

 Dr. Augustine Rukoma

Ukimwi  “upungufu wa kinga mwili”, ni ugonjwa unaoshambulia na kuua chembe chembe nyeupe za damu zinazosaidia mwili kupambana na magonjwa. Kutokana na upungufu huu wa kinga, magonjwa nyemelezi huanza kumpata muathirika wa ukimwi. Magonjwa yatokanayo na ukimwi uweza kujidhihirisha sehemu mbali mbali za mwili ikiwemo eneo la kinywa na uso. Kwa sasa nitaandika juu ya magonjwa ya eneo la kinywa na uso.
1. Fangasi za mdomoni (oral candidiasis)
Ugonjwa huu hujidhihirisha kama utando mweupe kwenye ulimi, paa la kinywa au kuta za kinywa, utando huu ni rahisi kukwanguliwa na kuacha ngozi laini yenye vipele vipele vyekundu. Wakati mwingine uonekana kama vipele vipele vyeupe kwenye kinywa.

picha hizi mbili hapa chini zinaonyesha fangasi kwenye paa lakinywa na kwenye ulimi

Matibabu: Ugonjwa huu hutibika kwa kutumia dawa za kawaida za fangasi, ziwe vidonge, za maji au za kumun’gunya katika hali ya gel

  












2. Kaposi’s sarcoma
Hii ni kansa itakanayo na chembe chembe zinazotengeneza ngozi ya ndani ya mishipa ya damu.
Kansa hii ilikuwepo tangu zamani lakini imeongezeka kwa kasi baada ya kugundulika kwa Ukimwi. Tafiti nyingi kwa sasa zinaonyesha kansa hii ina uhusiano mkubwa na Ukimwi.
Kansa hii kwenye kinywa inajidhihirisha kama uvimbe tepetepe wenye rangi ya zambarau japo wakati mwingine nyekundu damu ya mzee.
Wakati mwingine yawezekana usiwe uvimbe bali eneo fulani la ngizi zilizo tanda kinywa kubadilika rangi na kuwa zambarau au nyekundu.
Kansa hii inaweza jitokeza sehemu yoyote mdomoni, kama kwenye ulimi, kuta za kinywa, paa la kinywa na kwenye fizi na hata kwenye tonsili.
Nje ya kinywa kwenye uso, kansa hii hushambulia mitoki iliyo chini ya kidevu na kwenye shingo. Mitoki uvimba bila sababu ilyo wazi (kwa kawaida mitoki uvimba kama kuna kidonda sehemu fualani au ugonjwa).
Matibabu: Kwa wagonjwa wa Ukimwi kansa hii ikijitokeza ni miongoni wa sababu za kuanza kutumia dawa za kupunguza makali ya Ukimwi hata kama kinga yako bado iko juu. Matibabu yanaweza kuwa upasuaji kuondoa uvimbe, mionzi kuunguza chembe chembe za kansa, dawa za kansa au muunganiko wa njia njia mbili kati ya hizo au zote kwa pamoja.

picha chini ikionyesha kapos's sarcoma ya kwenye fizi

3. Magonjwa ya fizi
Kwa kawaida magonjwa ya fizi huwapata watu wasiopiga mswaki au wanaopiga mswaki isivyo paswa. Mara nyingi utakuta mtu mwenye magonjwa haya meno yakiwa na tando za uchafu na wadudu (dental plaque) au hata ugaga uliojishikiza kwenye meno kama miamba (calculus). Lakini kwa mgonjwa wa ukimwi waweza kuta kinywa ni kisafi lakini fizi zimejaa vidonda vidonda, na vidonda hivi husambaa kwa kasi.
Magonjwa haya fizi hushambulia pia mifupa inayoshikilia mizizi ya meno hivyo kupelekea meno kulegea na hatimaye kutoka
Matibabu: Kusafisha meno na kutumia dawa za antibiotic za kusukutua na vidonge vya kumeza.

4. Kuvimba kwa tezi kubwa la mate lililopo jirani na sikio (parotid salivary gland enlargement)
Huku ni kuvimba hadi kuonekana kwa tezi la mate lililopo jirani ya sikio. Kwa kawaida tezi ili halionekani, hivyo ukiliona limevimba jua kuna tatizo. Ugonjwa huu huenda sambamba na kukauka kwa kinywa, kwani matezi haya ndiyo hutoa kiwango kikubwa cha mate mdomoni. Unaweza kuvimba tezi la upande mmoja au pande zote mbili.
Matibabu: Ugonjwa huu huweza kujiponea wenyewe lakini wakati mwingine yaweza kuhitaji matibabu.

5.    Kuvimba kwa mitoki ya maeneo chini ya kidevu na shingo
Kama nilivyokwisha sema hapo juu, katika hali ya kawaida mitoki haionekani na wala huwezi kuihisi kwa kugusa. Ukiweza kuiona kwa macho kuwa imevimba au hata ukaweza kuihisi kwa kugusa hiyo ni dalili kwamba mitoki imevimba. Mbali ya majeraha na vidonda eneo la kinywa na uso mitoki hii pia huweza kushambuliwa na kansa ya karposi’s sarcoma au hata TB, lakini wakati mwingine inavimba tu bila sababu zilizo wazi.
Matibabu: Mitoki hii uweza kupona bila matibabu, lakini wakati mwingine matibabu yanatakiwa
Muhimu
Magojwa yote niliyotaja hapo juu yalikuwepo kabla ya Ukimwi isipokuwa yameongezeka baada ya Ukimwi kuingia, hivyo si kila mwenye magonjwa hayo ana Ukimwi. Kimsingi wagonjwa walio wengi wenye magonjwa hayo wana virusi vya Ukimwi.
Katika utumishi wangu, ukiondoa fangasi za mdomoni, wagonjwa wote niliowatibu na wakakubali kupima wote waligundulika wana Ukimwi. Lakini nasisitiza si lazima mwenye magonjwa hayo awe na Ukimwi.
 Kwa makala zaidi, maswali na ushauri mtembelee kwenye blog yake ya http://rukomadentalanswers.blogspot.com hii ni kwa lugha ya kiingereza

Friday 14 October 2011

MATIBABU YA MENO YALIYOJIPANGA VIBAYA (ORTHODINTIC TREATMENT)

Baadi ya watu wana meno yaliyojipanga visivyo. Katika hali ya kawaida meno yanatakiwa yawe katika mahusiano mazuri kiasi kwamba meno ya juu yaweze kukutana vizuri na yaliyo jirani yakae vizuri pia. Utakuta baadhi ya watu meno ya juu yamechomoza mbele sana kiasi kwamba hata kufunga mdomo ni tatizo, wengine ya chini kuvutika mbele zaidi na kuwa na kidevu kilichochongoka kwenda mbele na wengine yamepandana pandana. Mpangilio mbaya wa meno unaweza kuwa mbaya zaidi kiasi cha kumugasi mhusika na wakati mwingine meno yenyewe kushindwa kufanya kazi zake vizuri. Taizo linguine la meno yalijipanga vibaya ni vigumu kuyasafisha na hivyo kuyaweka meno katika hatari ya kuoza na kusababisha magonjwa ya fizi.
Nini kinasababisha matatizo haya?
·         Maumbili yatokanayo na vinasaba na uridhi
·         Tabia kama kunyionya vidole utotoni hata ukubwani kwa wengine
·         Kuwahi kutoka meno ya utotoni
·         Kuchelewa kutoka kwa mano ya utotoni hivyo kuyafanya ya ukubwani kuota upande
·         Ajari wakati wa kujifungua ambayo inaweza kuadhiri maeneo ya kukua kwa taya
Matibabu-lengo kubwa la matibabu ni kuyaweka meno katika mpangilio unaokubalika, ili kuboresha muonekano, utafunaji na hata utamkaji wa maneno.
Matibabu huusisha kuwekewa nyaya kwenye meno ambazo husaidia kuyavuta na kuyaweka katika mpangilio mzuri. Nyaya zaweza kuwa za kufunga moja kwa moja kwa vifaa maalumu na kuwa vinafanyiwa marekebisho kadri meno yanavyozidi kujipanga (fixed orthodontic appliances); lakini pia nyaya hizi zaweza kuwa za kuvaa na kuondoa kadri mgonjwa anavyotaka (removable orthodontic appliances). Kama mpangilio ni mbaya zaidi, ili kufanikisha matibabu haya, yawezekana baadhi ya meno kuondolewa ili kutoa nafasi kwa yaliyobaki kujipanga.
 Muda wa kuvaa nyaya hizi yaweza kuwa miezi sita au zaidi kulingana na ukubwa wa tatizo na wakati mwingine ushirikiano wa mgonjwa.
Muda mzuri wa kufanya matibabu haya ni pale ambapo mtoto bado anakuwa anakua (chini ya miaka 18). Zaidi ya umri huu matibabu huwa magumu, kuchukua muda mrefu na wakati mwingine kutoa matokeo ambayo hayaridhishi.
Kwa wale ambayo matatizo haya yanatokana na mojawapo ya mataya kuwa dodo kuliko kawaida au kunyume chake basi upasuaji unatakiwa kupunguza au kuongeza taya husika.
Ni vizuri kuwaangalia watoto wetu mara kwa mara, kwani matibabu ni rahisi yakigundulika mapema.
Msisitizo tembelea kliniki ya meno wewe pamoja na familia yako angalau mara mbili kwa mwaka. Kumbuka matibabu ya meno ni gharama na bima nyingi zinayakimbia. Tiba ya mapema ni sawa na kinga.
Picha hapo chini zinaonyesha mgonjwa kabla, wakati na baada ya matibabu
Kabla ya matibabu
Wakati wa matibabu


Baada ya matibabu

KULIKA KWA MENO (TEETH WEAR)

Na Dr. Augustine Mbehoma Rukoma
Hii ni hali ya ambapo sehemu ngumu ya nje ya meno uondoka na kusababisha sehemu ya ndani kuwa wazi. Tatizo hili huanza kwa kuondoka sehemu ngumu ya nje (enamel) na kuiweka wazi sehemu ya kati ambayo ni ngumu pia (dentine). Tatizo likiendelea bila matibabu hufanya kiini cha jino ambako kuna mishipa ya damu, mishipa ya fahamu na chembe chembe mbali kuwa wazi (dental pulp exposure).
Dalili hutegemea na kiwango cha ulikaji. Kama ni sehemu ya nje kabisa imetoka, dalili uweza kuwa msisimuko (sensitivity) wakati wakunywa vinywaji vya baridi, vya sukari na hata upepo ukiyapuliza meno. Kama kiini cha jino kitakuwa wazi basi maumivu uanza na yanaweza kuwa makali kabisa.
Matibabu hutegemea kiwango cha uharibifu. Kama uharibifu ni kidogo utumiaji wa dawa za meno zenye madini zaidi hasa ya fluoride (magaddi?) inaweza kuondoa dalili, wakati mwingine kutumia dawa za kupaka kitaalam, kuziba na kuvalisha kofia ngumu (crown) meno husika na mwisho ni kufanya matibabu ya mzizi wa jino (root canal treatment) au kung’oa jino kama kiini cha jino kimebaki wazi.
Ziko aina mbali mbali za kulika kwa meno kutokana na nini kinasababisha tatizo, na kinga au tiba hutegemea nini kisababishi.
Kusagika kwa meno (attrition)
Huku ni kulika kwa meno kwenye sehemu ambapo meno ya juu na chini hukutana (occlusal surfaces). Katika hali ya kawaida meno hulika sehemu hizi kutokana na kadri yanavyoendelea kutumika kusaga vyakula, hali hii uendelea polepole kadri mtu anavyoendelea kuishi (umri) kitaalamu inajulikana kama phyisiological attrition. Si rahisi kuhisi dalili zake kwani mwili hujaribu kuzipa vitundu vya mifereji midogo inayotoka kwenye kiini cha jino kwenda kwenye sehemu ngumu ya kati (dentine). Ni vitundu hivi ambavyo vikiwa wazi husababisha msisimko (sensitivity). Kulika kwa meno sehemu ya kusaga unakuwa ugonjwa pale unapotokana na mambo mengine zaidi ya kule kwa kawaida kwa kuongeza umri
Baadhi ya matatizo yanayosababisha hali
1.      Kusaga meno (bruxism)- hii ni hali ambayo mtu husaga meno yake wakati hatafuni kitu chochote na mara nyingi mtu huwa hajitambui kama ana tatizo hili. Hali hii mara nyingi hujitokeza wakati wa usiku mtu akiwa amelala (nocturnal bruxism) japo kwa wachache wanaweza saga mchana pia. Si rahisi mtu wa namana hii kujitambua mpaka pale atakapoambiwa na mtu wanayelala pamoja au atakapo kwenda kwa mtaalamu wa meno na kuelezwa.

Nini husababisha hali hii
Yapo baadhi ya mambo yanayoweza kusababisha tatizo hili na zaidi inahusishwa na mabadiliko ya ki saikologia. Watu wenye mawazo mengi wanaonekana kuwa kwenye hatari zaidi ya kupatwa na tatizo hili.

Tatizo hili pia linaweza kutokana na jino lililozibwa na kujazwa zaidi ya kwaida. Mwili hufanya harakati za kupungu sehemu ilyozidi kwa kuisaga na hatimaye kujikuta umejenga mazoea, kiasi kwamba hata jino likisha kuwa levo bado unaendelea kusaga tu.

Pia wale wanaokaa kwenye meza kwa muda mrefu wakisoma au vyovyote huku wameshikiria kidevu kwa nguvu, nao ni wahanga wa ungonjwa huu. Katika hali ya kawaida mtu ukiwa umefunga mdomo umetulia meno ya juu na ya chini huwa hayakutani bali huacha nafasi kama milimita mbil hivi (resting space). Sasa ukiyabana pamoja kwa muda mrefu kwa kushikilia kidevu, utayafanya yajenge mazoea kuyakushikana hata pale ambapo hujashika kidevu na mwishowe kuanza kusagana

Dalili zake na viashilia vyake ni mgonjwa mwenyewe kuhisi msisimko wakati wa kunywa vitu vya baridi, maumivu kama kiwango cha uharibifu ni kikubwa kiasi cha kukiacha kiini jino wazi (dental pulp exposure). Ukiangalia meno utakuta yamelika sehemu ya kutafunia kwa magego na visaidizi vyake (molars and premolars), sehemu sa kukatia na kuchoma kwa meno ya mbele (canines and incisors). Kusagika huanzia sehemu za meno zilizoinuka (cusps) ambazo hatimaye huondoka kabisa na kuwa flati. Meno huweza kusagika mpaka wakati mwingine kufikia kwenye levo ya fizi. Watu wenye tatizo hili huonekana wana uso wa mraba kutokana na msuli mkubwa wa kuvuta taya (masseter muscle) kunenepa kutokana na kutumika zaidi. Mgonjwa pia huweza kuchoka kirahisi misuri wakati wakutafuna katika hali ya kawaida.
Tatizo linaweza kuathili hata sehemu ya muunganiko wa taya la chini na fuvu (tempromandibular joint-TMJ). mgonjwa huweza kusikia maumivu kwenye jointi hii na wakati mwingine kufyatuka fyatuka (TMJ dislocation) au kutoa sauti wakati wakufungua na kufunga kinywa (popping or cricking sound in TMJ).












Picha zikionyesha meno yalisagika



Kwa chini; upande wa juu-kinachoonekana kama kuvimba shavu ni msuli wa kuvuta taya (masseter muscle) ulioongezeka ukubwa kutokana na kusaga meno. Picha ya chini mwezi mmoja baada ya kupata matibabu ya uhakika, msuli unarudi katika hali ya kawaida.

Matibabu –ni vizuri kujua chanzo cha tatizo hili na kukishughulia kwanza kabla ya kufanya matibabu zaidi ya meno kurekebisha uharibifu uliotaka na msagiko. Utafiti unaonye wengi wenye matatizo haya ni wenye mawazo yaliyo zidi kiwango (stress). Lazima hujue kwanini mtu anawaza sana ili umkancell au hata umpeleke kwa wataamu wa mambo hayo (psycologist) ili waweze kumsaidia.

Wakati hayo yakiendele inabidi kumfundisha mgonjwa kulegeza taya (relaxation exercise) na kuachanisha meno kila anapo hisi meno ya juu na ya chini yamekutana. Akifanya mazoezi haya kwa muda mrefu mwili huweza kujenga mazoea kuwa kila meno yakikutana yaachanishwe (conditioned reflex action). Mgonjwa akiacha kusaga basi matibabu ya kurekebisha madhara yanaweza kufanyika kwa mafanikio makubwa, iwe kuziba, kuua mzizi wa jino na kuyavalisha meno kofia ngumu hasa metal reinforced porcelain crown
Kwa wale ambao ni vigumu kuacha tabia ya kusaga wanaweza kutengenezewa kifaa maalumu cha kulinda meno wakati wa usiku (nigh guards), mgonjwa anava kifaa hiki usiku wakati wa kulala kuzuia meno kugusana na baada ya muda atazoea pia na kuacha kusaga. Kifaa hiki husaidia pia kuondoa matatizo yaliyokwisha jitokeza kwenye jointi.         
                                                                  


kifaa cha kukinga meno                                mgonjwa akiwa amevaa kifaa
yasisagane (night guard)


Ni vizuri kumuuliza mwenzako kama amewai kukusikia ukisaga meno usiku ili uweze kuchukua hatua za kuwaona wataamu mapema. Kumbuka kujua tatizo mapema na kulitibu ni sehemu ya hatua za kinga.