Thursday 20 October 2011

Yajue Baadhi ya Magonjwa Yenye Uhusiano Mkubwa na UKIMWI Katika Kinywa na Maeneo ya Uso

 Dr. Augustine Rukoma

Ukimwi  “upungufu wa kinga mwili”, ni ugonjwa unaoshambulia na kuua chembe chembe nyeupe za damu zinazosaidia mwili kupambana na magonjwa. Kutokana na upungufu huu wa kinga, magonjwa nyemelezi huanza kumpata muathirika wa ukimwi. Magonjwa yatokanayo na ukimwi uweza kujidhihirisha sehemu mbali mbali za mwili ikiwemo eneo la kinywa na uso. Kwa sasa nitaandika juu ya magonjwa ya eneo la kinywa na uso.
1. Fangasi za mdomoni (oral candidiasis)
Ugonjwa huu hujidhihirisha kama utando mweupe kwenye ulimi, paa la kinywa au kuta za kinywa, utando huu ni rahisi kukwanguliwa na kuacha ngozi laini yenye vipele vipele vyekundu. Wakati mwingine uonekana kama vipele vipele vyeupe kwenye kinywa.

picha hizi mbili hapa chini zinaonyesha fangasi kwenye paa lakinywa na kwenye ulimi

Matibabu: Ugonjwa huu hutibika kwa kutumia dawa za kawaida za fangasi, ziwe vidonge, za maji au za kumun’gunya katika hali ya gel

  












2. Kaposi’s sarcoma
Hii ni kansa itakanayo na chembe chembe zinazotengeneza ngozi ya ndani ya mishipa ya damu.
Kansa hii ilikuwepo tangu zamani lakini imeongezeka kwa kasi baada ya kugundulika kwa Ukimwi. Tafiti nyingi kwa sasa zinaonyesha kansa hii ina uhusiano mkubwa na Ukimwi.
Kansa hii kwenye kinywa inajidhihirisha kama uvimbe tepetepe wenye rangi ya zambarau japo wakati mwingine nyekundu damu ya mzee.
Wakati mwingine yawezekana usiwe uvimbe bali eneo fulani la ngizi zilizo tanda kinywa kubadilika rangi na kuwa zambarau au nyekundu.
Kansa hii inaweza jitokeza sehemu yoyote mdomoni, kama kwenye ulimi, kuta za kinywa, paa la kinywa na kwenye fizi na hata kwenye tonsili.
Nje ya kinywa kwenye uso, kansa hii hushambulia mitoki iliyo chini ya kidevu na kwenye shingo. Mitoki uvimba bila sababu ilyo wazi (kwa kawaida mitoki uvimba kama kuna kidonda sehemu fualani au ugonjwa).
Matibabu: Kwa wagonjwa wa Ukimwi kansa hii ikijitokeza ni miongoni wa sababu za kuanza kutumia dawa za kupunguza makali ya Ukimwi hata kama kinga yako bado iko juu. Matibabu yanaweza kuwa upasuaji kuondoa uvimbe, mionzi kuunguza chembe chembe za kansa, dawa za kansa au muunganiko wa njia njia mbili kati ya hizo au zote kwa pamoja.

picha chini ikionyesha kapos's sarcoma ya kwenye fizi

3. Magonjwa ya fizi
Kwa kawaida magonjwa ya fizi huwapata watu wasiopiga mswaki au wanaopiga mswaki isivyo paswa. Mara nyingi utakuta mtu mwenye magonjwa haya meno yakiwa na tando za uchafu na wadudu (dental plaque) au hata ugaga uliojishikiza kwenye meno kama miamba (calculus). Lakini kwa mgonjwa wa ukimwi waweza kuta kinywa ni kisafi lakini fizi zimejaa vidonda vidonda, na vidonda hivi husambaa kwa kasi.
Magonjwa haya fizi hushambulia pia mifupa inayoshikilia mizizi ya meno hivyo kupelekea meno kulegea na hatimaye kutoka
Matibabu: Kusafisha meno na kutumia dawa za antibiotic za kusukutua na vidonge vya kumeza.

4. Kuvimba kwa tezi kubwa la mate lililopo jirani na sikio (parotid salivary gland enlargement)
Huku ni kuvimba hadi kuonekana kwa tezi la mate lililopo jirani ya sikio. Kwa kawaida tezi ili halionekani, hivyo ukiliona limevimba jua kuna tatizo. Ugonjwa huu huenda sambamba na kukauka kwa kinywa, kwani matezi haya ndiyo hutoa kiwango kikubwa cha mate mdomoni. Unaweza kuvimba tezi la upande mmoja au pande zote mbili.
Matibabu: Ugonjwa huu huweza kujiponea wenyewe lakini wakati mwingine yaweza kuhitaji matibabu.

5.    Kuvimba kwa mitoki ya maeneo chini ya kidevu na shingo
Kama nilivyokwisha sema hapo juu, katika hali ya kawaida mitoki haionekani na wala huwezi kuihisi kwa kugusa. Ukiweza kuiona kwa macho kuwa imevimba au hata ukaweza kuihisi kwa kugusa hiyo ni dalili kwamba mitoki imevimba. Mbali ya majeraha na vidonda eneo la kinywa na uso mitoki hii pia huweza kushambuliwa na kansa ya karposi’s sarcoma au hata TB, lakini wakati mwingine inavimba tu bila sababu zilizo wazi.
Matibabu: Mitoki hii uweza kupona bila matibabu, lakini wakati mwingine matibabu yanatakiwa
Muhimu
Magojwa yote niliyotaja hapo juu yalikuwepo kabla ya Ukimwi isipokuwa yameongezeka baada ya Ukimwi kuingia, hivyo si kila mwenye magonjwa hayo ana Ukimwi. Kimsingi wagonjwa walio wengi wenye magonjwa hayo wana virusi vya Ukimwi.
Katika utumishi wangu, ukiondoa fangasi za mdomoni, wagonjwa wote niliowatibu na wakakubali kupima wote waligundulika wana Ukimwi. Lakini nasisitiza si lazima mwenye magonjwa hayo awe na Ukimwi.
 Kwa makala zaidi, maswali na ushauri mtembelee kwenye blog yake ya http://rukomadentalanswers.blogspot.com hii ni kwa lugha ya kiingereza

Friday 14 October 2011

MATIBABU YA MENO YALIYOJIPANGA VIBAYA (ORTHODINTIC TREATMENT)

Baadi ya watu wana meno yaliyojipanga visivyo. Katika hali ya kawaida meno yanatakiwa yawe katika mahusiano mazuri kiasi kwamba meno ya juu yaweze kukutana vizuri na yaliyo jirani yakae vizuri pia. Utakuta baadhi ya watu meno ya juu yamechomoza mbele sana kiasi kwamba hata kufunga mdomo ni tatizo, wengine ya chini kuvutika mbele zaidi na kuwa na kidevu kilichochongoka kwenda mbele na wengine yamepandana pandana. Mpangilio mbaya wa meno unaweza kuwa mbaya zaidi kiasi cha kumugasi mhusika na wakati mwingine meno yenyewe kushindwa kufanya kazi zake vizuri. Taizo linguine la meno yalijipanga vibaya ni vigumu kuyasafisha na hivyo kuyaweka meno katika hatari ya kuoza na kusababisha magonjwa ya fizi.
Nini kinasababisha matatizo haya?
·         Maumbili yatokanayo na vinasaba na uridhi
·         Tabia kama kunyionya vidole utotoni hata ukubwani kwa wengine
·         Kuwahi kutoka meno ya utotoni
·         Kuchelewa kutoka kwa mano ya utotoni hivyo kuyafanya ya ukubwani kuota upande
·         Ajari wakati wa kujifungua ambayo inaweza kuadhiri maeneo ya kukua kwa taya
Matibabu-lengo kubwa la matibabu ni kuyaweka meno katika mpangilio unaokubalika, ili kuboresha muonekano, utafunaji na hata utamkaji wa maneno.
Matibabu huusisha kuwekewa nyaya kwenye meno ambazo husaidia kuyavuta na kuyaweka katika mpangilio mzuri. Nyaya zaweza kuwa za kufunga moja kwa moja kwa vifaa maalumu na kuwa vinafanyiwa marekebisho kadri meno yanavyozidi kujipanga (fixed orthodontic appliances); lakini pia nyaya hizi zaweza kuwa za kuvaa na kuondoa kadri mgonjwa anavyotaka (removable orthodontic appliances). Kama mpangilio ni mbaya zaidi, ili kufanikisha matibabu haya, yawezekana baadhi ya meno kuondolewa ili kutoa nafasi kwa yaliyobaki kujipanga.
 Muda wa kuvaa nyaya hizi yaweza kuwa miezi sita au zaidi kulingana na ukubwa wa tatizo na wakati mwingine ushirikiano wa mgonjwa.
Muda mzuri wa kufanya matibabu haya ni pale ambapo mtoto bado anakuwa anakua (chini ya miaka 18). Zaidi ya umri huu matibabu huwa magumu, kuchukua muda mrefu na wakati mwingine kutoa matokeo ambayo hayaridhishi.
Kwa wale ambayo matatizo haya yanatokana na mojawapo ya mataya kuwa dodo kuliko kawaida au kunyume chake basi upasuaji unatakiwa kupunguza au kuongeza taya husika.
Ni vizuri kuwaangalia watoto wetu mara kwa mara, kwani matibabu ni rahisi yakigundulika mapema.
Msisitizo tembelea kliniki ya meno wewe pamoja na familia yako angalau mara mbili kwa mwaka. Kumbuka matibabu ya meno ni gharama na bima nyingi zinayakimbia. Tiba ya mapema ni sawa na kinga.
Picha hapo chini zinaonyesha mgonjwa kabla, wakati na baada ya matibabu
Kabla ya matibabu
Wakati wa matibabu


Baada ya matibabu

KULIKA KWA MENO (TEETH WEAR)

Na Dr. Augustine Mbehoma Rukoma
Hii ni hali ya ambapo sehemu ngumu ya nje ya meno uondoka na kusababisha sehemu ya ndani kuwa wazi. Tatizo hili huanza kwa kuondoka sehemu ngumu ya nje (enamel) na kuiweka wazi sehemu ya kati ambayo ni ngumu pia (dentine). Tatizo likiendelea bila matibabu hufanya kiini cha jino ambako kuna mishipa ya damu, mishipa ya fahamu na chembe chembe mbali kuwa wazi (dental pulp exposure).
Dalili hutegemea na kiwango cha ulikaji. Kama ni sehemu ya nje kabisa imetoka, dalili uweza kuwa msisimuko (sensitivity) wakati wakunywa vinywaji vya baridi, vya sukari na hata upepo ukiyapuliza meno. Kama kiini cha jino kitakuwa wazi basi maumivu uanza na yanaweza kuwa makali kabisa.
Matibabu hutegemea kiwango cha uharibifu. Kama uharibifu ni kidogo utumiaji wa dawa za meno zenye madini zaidi hasa ya fluoride (magaddi?) inaweza kuondoa dalili, wakati mwingine kutumia dawa za kupaka kitaalam, kuziba na kuvalisha kofia ngumu (crown) meno husika na mwisho ni kufanya matibabu ya mzizi wa jino (root canal treatment) au kung’oa jino kama kiini cha jino kimebaki wazi.
Ziko aina mbali mbali za kulika kwa meno kutokana na nini kinasababisha tatizo, na kinga au tiba hutegemea nini kisababishi.
Kusagika kwa meno (attrition)
Huku ni kulika kwa meno kwenye sehemu ambapo meno ya juu na chini hukutana (occlusal surfaces). Katika hali ya kawaida meno hulika sehemu hizi kutokana na kadri yanavyoendelea kutumika kusaga vyakula, hali hii uendelea polepole kadri mtu anavyoendelea kuishi (umri) kitaalamu inajulikana kama phyisiological attrition. Si rahisi kuhisi dalili zake kwani mwili hujaribu kuzipa vitundu vya mifereji midogo inayotoka kwenye kiini cha jino kwenda kwenye sehemu ngumu ya kati (dentine). Ni vitundu hivi ambavyo vikiwa wazi husababisha msisimko (sensitivity). Kulika kwa meno sehemu ya kusaga unakuwa ugonjwa pale unapotokana na mambo mengine zaidi ya kule kwa kawaida kwa kuongeza umri
Baadhi ya matatizo yanayosababisha hali
1.      Kusaga meno (bruxism)- hii ni hali ambayo mtu husaga meno yake wakati hatafuni kitu chochote na mara nyingi mtu huwa hajitambui kama ana tatizo hili. Hali hii mara nyingi hujitokeza wakati wa usiku mtu akiwa amelala (nocturnal bruxism) japo kwa wachache wanaweza saga mchana pia. Si rahisi mtu wa namana hii kujitambua mpaka pale atakapoambiwa na mtu wanayelala pamoja au atakapo kwenda kwa mtaalamu wa meno na kuelezwa.

Nini husababisha hali hii
Yapo baadhi ya mambo yanayoweza kusababisha tatizo hili na zaidi inahusishwa na mabadiliko ya ki saikologia. Watu wenye mawazo mengi wanaonekana kuwa kwenye hatari zaidi ya kupatwa na tatizo hili.

Tatizo hili pia linaweza kutokana na jino lililozibwa na kujazwa zaidi ya kwaida. Mwili hufanya harakati za kupungu sehemu ilyozidi kwa kuisaga na hatimaye kujikuta umejenga mazoea, kiasi kwamba hata jino likisha kuwa levo bado unaendelea kusaga tu.

Pia wale wanaokaa kwenye meza kwa muda mrefu wakisoma au vyovyote huku wameshikiria kidevu kwa nguvu, nao ni wahanga wa ungonjwa huu. Katika hali ya kawaida mtu ukiwa umefunga mdomo umetulia meno ya juu na ya chini huwa hayakutani bali huacha nafasi kama milimita mbil hivi (resting space). Sasa ukiyabana pamoja kwa muda mrefu kwa kushikilia kidevu, utayafanya yajenge mazoea kuyakushikana hata pale ambapo hujashika kidevu na mwishowe kuanza kusagana

Dalili zake na viashilia vyake ni mgonjwa mwenyewe kuhisi msisimko wakati wa kunywa vitu vya baridi, maumivu kama kiwango cha uharibifu ni kikubwa kiasi cha kukiacha kiini jino wazi (dental pulp exposure). Ukiangalia meno utakuta yamelika sehemu ya kutafunia kwa magego na visaidizi vyake (molars and premolars), sehemu sa kukatia na kuchoma kwa meno ya mbele (canines and incisors). Kusagika huanzia sehemu za meno zilizoinuka (cusps) ambazo hatimaye huondoka kabisa na kuwa flati. Meno huweza kusagika mpaka wakati mwingine kufikia kwenye levo ya fizi. Watu wenye tatizo hili huonekana wana uso wa mraba kutokana na msuli mkubwa wa kuvuta taya (masseter muscle) kunenepa kutokana na kutumika zaidi. Mgonjwa pia huweza kuchoka kirahisi misuri wakati wakutafuna katika hali ya kawaida.
Tatizo linaweza kuathili hata sehemu ya muunganiko wa taya la chini na fuvu (tempromandibular joint-TMJ). mgonjwa huweza kusikia maumivu kwenye jointi hii na wakati mwingine kufyatuka fyatuka (TMJ dislocation) au kutoa sauti wakati wakufungua na kufunga kinywa (popping or cricking sound in TMJ).












Picha zikionyesha meno yalisagika



Kwa chini; upande wa juu-kinachoonekana kama kuvimba shavu ni msuli wa kuvuta taya (masseter muscle) ulioongezeka ukubwa kutokana na kusaga meno. Picha ya chini mwezi mmoja baada ya kupata matibabu ya uhakika, msuli unarudi katika hali ya kawaida.

Matibabu –ni vizuri kujua chanzo cha tatizo hili na kukishughulia kwanza kabla ya kufanya matibabu zaidi ya meno kurekebisha uharibifu uliotaka na msagiko. Utafiti unaonye wengi wenye matatizo haya ni wenye mawazo yaliyo zidi kiwango (stress). Lazima hujue kwanini mtu anawaza sana ili umkancell au hata umpeleke kwa wataamu wa mambo hayo (psycologist) ili waweze kumsaidia.

Wakati hayo yakiendele inabidi kumfundisha mgonjwa kulegeza taya (relaxation exercise) na kuachanisha meno kila anapo hisi meno ya juu na ya chini yamekutana. Akifanya mazoezi haya kwa muda mrefu mwili huweza kujenga mazoea kuwa kila meno yakikutana yaachanishwe (conditioned reflex action). Mgonjwa akiacha kusaga basi matibabu ya kurekebisha madhara yanaweza kufanyika kwa mafanikio makubwa, iwe kuziba, kuua mzizi wa jino na kuyavalisha meno kofia ngumu hasa metal reinforced porcelain crown
Kwa wale ambao ni vigumu kuacha tabia ya kusaga wanaweza kutengenezewa kifaa maalumu cha kulinda meno wakati wa usiku (nigh guards), mgonjwa anava kifaa hiki usiku wakati wa kulala kuzuia meno kugusana na baada ya muda atazoea pia na kuacha kusaga. Kifaa hiki husaidia pia kuondoa matatizo yaliyokwisha jitokeza kwenye jointi.         
                                                                  


kifaa cha kukinga meno                                mgonjwa akiwa amevaa kifaa
yasisagane (night guard)


Ni vizuri kumuuliza mwenzako kama amewai kukusikia ukisaga meno usiku ili uweze kuchukua hatua za kuwaona wataamu mapema. Kumbuka kujua tatizo mapema na kulitibu ni sehemu ya hatua za kinga.

KUYEYUKA KWA MENO (TEETH EROSION)

Na Dr. Augustine Mbehoma Rukoma
Ziko aina mbali mbali za kulika kwa meno kulingana na nini kinasababisha tatizo. Aidha kinga au tiba hutegemea nini kinasababisha tatizo hilo. Leo nitaongelea aina nyingine ya kulika kwa meno
Kuyeyuka kwa meno (tooth erosion) ni kulika kwa meno kunakosababishwa na kemikali hasa tindikali. Tindikali inayoyeyusha meno haya yaweza kutoka nje au ndani ya mwili wenyewe.
  • Kuyeyuka kwa meno kunakosababishwa na tindikali toka nje ya mwili: Baadhi ya vyakula na vinywaji tunavyokula na kunywa vina kiwango kikubwa cha tindikali (acid), hivyo vyakula na vinywaji hivyo vikikaa kinywani kwa muda huweza kusababisha meno kuyeyuka. Kiwango cha uharibifu kinategemea mara ngapi unatumia vyakula/vinywaji hivyo, kiwango cha tindikali katika vinywaji hivyo na muda vinaokaa kinywani. Tindikali nyingine inaweza kupatikana katika hewa hasa maeneo ya viwanda vinavyotengeneza betri. Myeyuko unaotokana na tindikali ya nje huathiri zaidi sehemu za nje za meno (buccal or facial surfaces).  


 kuyeyuka kwa kweno kunakotokana na vinywaji vyenye tindikali

Watu walio katika hatari zaidi ya kupata tatizo hili ni wale ambao hunywa vinywaji vyenye kaboni kwa wingi (carbonated drinks), juice ya limau au wale wenye tabia ya kufyonza limau. Tatizo linaongezeka kwa wale wenye tabia ya kuweka juice na kukaa nayo mdomoni kwa muda bila kuimeza (unaisikilizia utamu mpaka kwenye kisogo). Unashauriwa unapokunywa juice hizi kumeza haraka.myeyuko utakanao na vinywaji vyatindikali
  • Kuyeyuka kwa meno kunakosababishwa na tindikali toka ndani ya mwili: Kuyeyuka huku kunasababishwa na tindikali kutoka kwenye tumbo. Meno yanakwanguka sehemu za ndani (palatal and lingual surfaces) kama picha inavyoonesha hapa kulia.

                    kuyeyuka kwa meno kunakosababishwa na tindikali toka ndani ya mwili


Watu watu walio katika hatari kubwa ya kupata tatizo hili ni wale ambao wana matatizo ya kutapika mara kwa mara kama ugonjwa sugu na wale ambao hula sana lakini kwa vile wanataka wabaki wembamba (slim), kila wakila baada ya muda hujitapisha ili wasinenepe. Matapishi huja na tindikali iliyoko tumboni (gastric hydrochloric acid). Wanywa pombe kali sugu nao hawaachwi nyuma, pombe kali hukwangua kuta za tumbo na kusabisha chronic gastritis hali ambayo tindikali huwa inamwagika kwenye tumbo zaidi ya kawaida na wakati mwingine hurudi kinywani kama mvuke na kusababisha madhara haya.

Hali inakuwa mbaya kwa wale wanao tapika mara kwa mara na katika hali ya kurudisha maji mwilini maana wanakuwa na kiu ya mara kwa mara hunywa juice au soda kwa wingi pia ili kukata kiu. Watu wa aina hii meno yao huyeyuka sehemu zote yaani nje na ndani.
Dalili
Katika hali zote eneo lililoathirika huonekana angavu, gumu, la njano kuelekea kahawia na laini (smooth).
Dalili zake ni kama zile za kulika kwa meno kunakotokana na namna nyingine, msisimko (sensitivity) wakati wa kunywa vinywaji baridi, kuvuta hewa na hata maumivu kulingana na kiwango cha uharibifu na uwezo wa mwili kujihami.
Matibabu

Matibabu hulenga kugundua na kutibu kisababishi. Kama ni matatizo ya tumbo tabibu wa meno atakupeleka kwa tabibu wa kawaida (general practitioner/physician). Kwa wale wenye tabia hatarishi, la msingi ni kushauriwa kuacha tabia hizo. Mgonjwa akitengemaa basi sehemu zilizoathirika huweza kupigwa viraka kwa dawa zenye rangi kama ya jino (composite veneer).
Kwa wale walioshindikana meno huvalishwa kofia ngumu (crown) ili kuyakinga na myeyuko zaidi.

Kuoza kwa meno (Dental Caries) ni ugonjwa wa kuambukiza

Dr. Augustine Mbehoma Rukoma 
Miaka ya nyuma iliaminika ugonjwa wa kuoza kwa meno si wa kuambukiza; lakini tafiti nyingi zilizofanyika zimethihilisha ni ugonjwa wa kuambukiza. Jino lililooza linaweza kuambukiza meno yaliyogusana nalo na pia mgonjwa aliyeoza meno au mwenye wadudu wanaosababisha kuoza kwa meno anaweza kuambukiza mwenzake/wenzake.
Wadudu wanaosababisha kuoza kwa meno ni sehemu ya wadudu wakazi kinywani (oral flora). Wadudu hawa hujishikiza kwenye meno na kufanya utando, wana uwezo wa kuchachua vyakula hasa vyenye asili ya sukari na kutoa tindikari. Ni tindikali hii ambayo huvuta madini kwenye meno na kuweka matobo. Utando huu wa wadudu kwenye jino moja unaweza kuwa na wadudu nusu biliononi, miongoni mwake ikiwemo jamii ya  mutans streptococci ambao kimsingi ndio wasababishaji wakuu wa kuoza meno. Waduduwengine ni kama Lactobacillus na Actinomyces
Namna ya kuambukiza-ndani ya jamii ya wadudu hawa ziko jamii zingine ndogondogo ambazo zinatofautiana kwa uwezo kuchachua vyakula na kutoa tindikali na hata uwezo wa kujishikiza kwenye meno. Kwa mtu mwenye wadudu wasio wakali anaweza kuambukizwa na mwenzake mwenye wadudu wakali na hivyo kuingia kwenye hatari zaidi ya kuoza meno. Tafiti zimeonyesha wapenzi/wanandoa kwa njia ya kubusiana wanaweza kuambukizana kwa njia hii. Watoto wanaochangia ice cream/ice water mashuleni pia wanaambukizana kwa njia hii. Tafiti pia zimeonyesha wazazi wanaotafunia vyakula watoto wao kama sehemu ya kuvilainisha wanaambukiza pia.
Njia nyingine ni jinolililooza kuambukiza menzake linayogusana nayo, tindikali inayozalishwa na wadudu katika jio lililooza linaweza kuathili lililo jirani. Ndio maana inashauriwa ukiona jino limeanza kuoza muone mtaalamu akalitibu au akaling’oe kama alitibiki ili lisiambukize mengine.
Namna ya kujikinga-
·         Njia muhimu ni kutembelea cliniki za meno angalau kila baada ya miezi sita
·         Kuzuia watoto kuchangia vyakula mudomoni
·         Kupima kuangalia kiwango na aina za bakiteria zilizi kwenye mate yake na kupata dawa ikibidi.
·         Kuhusu kubusiana sina la kusema

KUOZA KWA MENO MENGI KWA KASI KWA WATOTO WADOGO (RAMPANT CARIES IN CHILDREN)

Dr. Augustine Mbehoma Rukoma
DDS, MDent (Restorative Dentistry)
Tafsiri  ya neon “rampant caries” ni nyingi katika fani ya meno lakini la msingi ni kuoza kwa meno kunako enea kwa kasi na kuharibu vichwa (crowns) vya meno mengi au yote yaliyoota. Hii ni hali mbaya ya kuoza kwa meno ambayo hushambulia zaidi meno ya utotoni (milk teeth or primary dentition), japo wakati mwingine hata ukubwani.
Ugonjwa huu unajidhihilisha kwa kuanza na kuongezeka kwa kasi na kwa namna unavyo yashambulia meno na vyanzo vyake. Meno ushambuliwa kwa mpigo hasa kuanzia meno ya juu mbele, meno ya chini mbele ni mara chache kushambuliwa kwa vile yanakingwa na visababisha vya kuonza na ulimi.  Ugonjwa huu ushambulia hata maeneo ya meno ambayo kwa hali ya kawaida si rahisi kuoza, kama sehemu ya kukatia kwa meno ya mbele (icisal edges) na sehemu ya mbele kati na nyuma kati (facial and lingual surfaces).
Vijino vilivyo athilika uonekana brauni au vyeusi kama mkaa


 meno yaliyooza kwa wingi na kwa kasi yakiwa na rangi nyeusi
     meno yaliyooza yakiwa na rangi ya brown      
Nini husababisha meno kuoza kwa kasi utotoni?
Nadharia nyingi zinaonyesha kuna uhusiano mkubwa kati ya ugonjwa huu na tabia ya ulaji ya mtoto (feeding habits). Mfano kisababishi kikubwa ni watoto kunywa vinywaji vyenye sukari kwa muda mrefu na mara nyingi kwa kutumia chupa za kufyonzea (nursing bottles) ndio maana ugojwa huu wakati mwingine huitwa nursing bottle caries. Hii hujitokeza haswa kwa watoto wanaochwa na yaya zao, ambao huwapa vinywaji hivyo kila wanapohitaji au wakilia. Pamoja na kwamba ugonjwa huu hutokana zaidi na chupa za kufyonzea, japo mara chache lakini pia yawezekana kutokana na mama kumnyonyesha mtoto mara kwa mara au tuseme kila anapo hitaji; vile vile wale akina mama ambao hawataki usumbufu usiku hivyo kutumbukiza nyonyo zao kwenye vinywa vya watoto na wao kujilalia, hapa mtoto hujinyonyea usiku kucha hali hii kitaalamu hujulikana kama at will breast feeding.
Watoto walio katika hatari ya kupata ugonjwa huu
·         Watoto wa masikini ambao hawapigi mswaki kwa kizingizio cha kwamba mtoto ni mdogo, kumbuka meno ya utotoni yana madini kidogo
·         Watoto wa wafanyakazi wanashinda maofisini wakati wa kunyonyesha na waacha watoto kutumia chupa za kufyonzea kwa muda mrefu ambao hawapo nao
·         Watoto wagonjwa sugu wanaotumia dawa zenye sukari (syrups) mara kwa mara.
·         Watoto wanaoachwa kunyonyeshwa mapema na hivyo kutumia chupa kama  mbadala

Namna ya kumkinga mtoto wako
·         Punguza matumizi ya chupa za kufyonzea
·         Msipende kuwanyonyesha watoto kila wanapotaka hivyo, hasa kunyonyesha inapotumika kama njia ya kupoza mtoto anayelia
·         Jenga tabia ya kuwakagua watoto vinywani mara kwa mara na ukiona tatizo mpeleke hospitali mapema
·         Wasaidieni watoto kupiga mswaki mara baada ya meno kuanza kuota
·         Dhibiti matumizi ya vinywaji na na vitu vya sukari mara kwa mara
·         Msipende kuwapa watoto wadogo fedha kwani matumizi yake ni pipi na ice water au vinavyo fanana na hivyo
Matibabu
·         Kuziba meno yanayoweza kuzibika
·         n’goa yanayouma na hayawezi kuzibika na kutumia vitunza nafasi (space maintainers).
·         Acha yasiyoweza kuzibika lakini hayaumi yatatoka wakati wake ukifika
·         Pakaza madini ya fulolini kwa watoto walio katika hatari kubwa



mtoto akifyonza chupa

Wednesday 12 October 2011

KUYAFANYA MENO YENYE RANGI KWA MEUPE

Na Augustine Mbehoma Rukoma-DDS, MDent (Restorative Dentistry)
Wakati wa mwongo uliopita mahita ya kuboresha muonekano au kulembesha meno yameongezeka kwa kiwango kikubwa hasa katika nchi zilizo endelea, hii imechochewa na kupatikana chemikali za meno mpya (dental meterials) na vifaa kwa kasi ikiendana na kuboresha vile vya zamani. Sehemu nyingine iliyosababisha madaktari na mainginia wa meno ku
kuyafanya meno kuwa meupe ni se hemu ya fani ya taaluma ya meno chini ya ulembeshaji wa meno, fani hii jihusisha na boresha muonekano wa meno hasa hasa yale yanayo onekana wakati wa kutabasamu na kuongea. Inahusisha matibabu kama kuyafanya meno yenye rangi kuwa meupe, kunyoosha meno yaliyojipanga vibaya pamoja na kukarabati meno yaliyovunjika na yale yaliyoumbika visivyo (malformed teeth). Huko uingereza na sehemu nyingine za magharibu wanawake waliowengi wanatumia maelfu ya paundi/euro kuboresha mwonekano wa meno yao ali ambayo na huku inaanza kuingia
 Nini husababisha meno kugeuka rangi?
Meno kugeuka rangi husabishwa ni kimojwapo au muunganiko wa vitu vifutavyo: -
1. Vyakula na vinywaji kama vile vinyaji vyenye kaboni, wine na sigara.
2. Utumiaji wa maji yenye kiwango cha juu cha madini aina ya magadi (fluoride)  na utuumiaji wa magadi katika kulainisha vyakula katika kupika vyakula vigumu kama maharage na makande. Utafiti uliofanyika tanzani na Prof. Mabelya na wenzake umeonyesha kuwa kubadilika kwa rangi kutokana magadi kwa kiwango kikubwa ni kutumia magadi katika mapishi  ya vyakula hasa makande kule moshi kuliko ilivyo kwa maji.
3. Maumbile yasiyo sahihi ya sehemu ngumu za jino (enamel and dentine defects). Sehemu ngumu ya meno kama imeumbwa ikiwa laini ni rahisi kufyonza rangi na jino kuuota likiwa limegeuka rangi au kugeuka baada ya kuota.
4. Matumizi ya madawa kwa mama mjamzito ambaye tayari meno ya mtoto aliye tumboni yameanza kuumbwa lakini hayajapata madini ya kutosha na hata watoto wachanga ambao meno yao hayajakomaa. Systemic drugs such as tetracycline when taken during pregnancy or early child may be absorbed developing teeth buds which are not yet or less mineralized. 5. Kufa kwa kiini cha jino hasa kutoka na kujigonga wakati wa ajari au kupigana ngumi usoni (pulp necrosis), jino likigongwa mkwa nguvu damu huvuja ndani ya kiini cha jino na baadae huchachuliwa na kuto chemikali ambayo hupenya kwenye vitundu vidogo vodogo kwenye dentine na kujidhihilisha kama brown, zambarau au hata nyeusi. Hali hii yaweza tokea mapema baada ya kupata ajari lakini wakati mwingi inaweza kuchukua miaka kadhaa hata arobaini wakati mtu hakumbuki kuwa alitwangwa ngumi.

Kuyafanya meno yenye rangi yasimpendeza mwenye nayo kuwa meupe
(Bleaching or teeth whitening)
Kuhu ni kuyafanya meno yenye rangi kuwa meupe au kuongeza weupe wa yale yenye rangi ya kawaida kufikia kiwango cha weupe atakacho muhitaji kwa kutumia chemikali maalumu. Rangi ya kawaida ya meno kwa walio wengi ni uweupe kama wa maziwa (milky white). Rangi yeyote nje ya hiyo ni si ya kawaida (abnormal color or discoloration).
Kuwa na rangi isiyo ya kwaida hasa kwa meno ya mbele linaweza kuwa tatizo kubwa la urembo na kumsumbua mhusika kisaikolojia. Kuyafanya meno kuwa meupe kumelenga kuwaondelea wahusika tatizo hili japo mafanikio yake yanategemea kiwango rangi isiyo ya kawaida.
Kufanya meno kuwa meupe kwa kutumia chemikali, kunaweza kubadili yaliyo na rangi isiya ya kawaida kutoka yale yaliyoathilika kwa kiwango kidogo mpaka cha kati.  
Kufanya meno yawe meupe kwa kutumia chemikali uunguza (ixidises) rangi na kuiondoa. Chemikali zinazotumika   zina hydrogen peroxide 30%-35% na baadhi carbamide peroxide 10%. Chemikali hizi huweza kuondoa rangi zilizo sababishwa na vyakula, vinnywaji dawa za tetracycline, rangi kidogo iliyotokana na utumiaji wa madini ya magadi kwenye vyakula au kwenye maji (mild fluorosis) na mmeno yenye rangi ya yellow au grey itokanayo na umri kwenda. Inaweza kuondoa rangi itokanayo na uvutaji wa sigara na matumizi ya ugoro. Kwa wavutaji wa sigara sharti waache watumiapo chemikali hizi kwani muunganiko hydrogen peroxide na chemikali zilizopo kwenye moshi wa sigara unakisiwa kuongeza madhara ambayo tayari moshi wa sigara unasababisha kwenye mwili wa binadamu. Akina mama wanaonyosha haishauliwi pia pamoja na kwamba hakuna madhara ambayo yanajulikana mpaka sasa. 
kuboresha weupe wa meno kutumia chemikali


Kupiga meno viraka (Veneering)
Hii hufanyika kwa kuondoa sehemu ndogo ya juu ya jino kwenye enamel kama 0.5-1mm na baadae kupandika dawa yenye rangi nyeupe kulingana na mgonjwa anavyotaka mwenyewe.
Picha sikonyesha meno yaliyobadlika rangi kutokana na magadi kabla na baada ya kupigwa viraka


picha ya juu, meno yaliyoathilika na magadi kabla ya kupigwa viraka wakati ya chini ni baada ya kupigwa viraka (veneer)

Kumbuka: kuna rangi zaidi ya 26 nyeupe ambazo miongoni mwake mgonjwa anaweza kuchagua anayoitaka