Wednesday 12 October 2011

KUYAFANYA MENO YENYE RANGI KWA MEUPE

Na Augustine Mbehoma Rukoma-DDS, MDent (Restorative Dentistry)
Wakati wa mwongo uliopita mahita ya kuboresha muonekano au kulembesha meno yameongezeka kwa kiwango kikubwa hasa katika nchi zilizo endelea, hii imechochewa na kupatikana chemikali za meno mpya (dental meterials) na vifaa kwa kasi ikiendana na kuboresha vile vya zamani. Sehemu nyingine iliyosababisha madaktari na mainginia wa meno ku
kuyafanya meno kuwa meupe ni se hemu ya fani ya taaluma ya meno chini ya ulembeshaji wa meno, fani hii jihusisha na boresha muonekano wa meno hasa hasa yale yanayo onekana wakati wa kutabasamu na kuongea. Inahusisha matibabu kama kuyafanya meno yenye rangi kuwa meupe, kunyoosha meno yaliyojipanga vibaya pamoja na kukarabati meno yaliyovunjika na yale yaliyoumbika visivyo (malformed teeth). Huko uingereza na sehemu nyingine za magharibu wanawake waliowengi wanatumia maelfu ya paundi/euro kuboresha mwonekano wa meno yao ali ambayo na huku inaanza kuingia
 Nini husababisha meno kugeuka rangi?
Meno kugeuka rangi husabishwa ni kimojwapo au muunganiko wa vitu vifutavyo: -
1. Vyakula na vinywaji kama vile vinyaji vyenye kaboni, wine na sigara.
2. Utumiaji wa maji yenye kiwango cha juu cha madini aina ya magadi (fluoride)  na utuumiaji wa magadi katika kulainisha vyakula katika kupika vyakula vigumu kama maharage na makande. Utafiti uliofanyika tanzani na Prof. Mabelya na wenzake umeonyesha kuwa kubadilika kwa rangi kutokana magadi kwa kiwango kikubwa ni kutumia magadi katika mapishi  ya vyakula hasa makande kule moshi kuliko ilivyo kwa maji.
3. Maumbile yasiyo sahihi ya sehemu ngumu za jino (enamel and dentine defects). Sehemu ngumu ya meno kama imeumbwa ikiwa laini ni rahisi kufyonza rangi na jino kuuota likiwa limegeuka rangi au kugeuka baada ya kuota.
4. Matumizi ya madawa kwa mama mjamzito ambaye tayari meno ya mtoto aliye tumboni yameanza kuumbwa lakini hayajapata madini ya kutosha na hata watoto wachanga ambao meno yao hayajakomaa. Systemic drugs such as tetracycline when taken during pregnancy or early child may be absorbed developing teeth buds which are not yet or less mineralized. 5. Kufa kwa kiini cha jino hasa kutoka na kujigonga wakati wa ajari au kupigana ngumi usoni (pulp necrosis), jino likigongwa mkwa nguvu damu huvuja ndani ya kiini cha jino na baadae huchachuliwa na kuto chemikali ambayo hupenya kwenye vitundu vidogo vodogo kwenye dentine na kujidhihilisha kama brown, zambarau au hata nyeusi. Hali hii yaweza tokea mapema baada ya kupata ajari lakini wakati mwingi inaweza kuchukua miaka kadhaa hata arobaini wakati mtu hakumbuki kuwa alitwangwa ngumi.

Kuyafanya meno yenye rangi yasimpendeza mwenye nayo kuwa meupe
(Bleaching or teeth whitening)
Kuhu ni kuyafanya meno yenye rangi kuwa meupe au kuongeza weupe wa yale yenye rangi ya kawaida kufikia kiwango cha weupe atakacho muhitaji kwa kutumia chemikali maalumu. Rangi ya kawaida ya meno kwa walio wengi ni uweupe kama wa maziwa (milky white). Rangi yeyote nje ya hiyo ni si ya kawaida (abnormal color or discoloration).
Kuwa na rangi isiyo ya kwaida hasa kwa meno ya mbele linaweza kuwa tatizo kubwa la urembo na kumsumbua mhusika kisaikolojia. Kuyafanya meno kuwa meupe kumelenga kuwaondelea wahusika tatizo hili japo mafanikio yake yanategemea kiwango rangi isiyo ya kawaida.
Kufanya meno kuwa meupe kwa kutumia chemikali, kunaweza kubadili yaliyo na rangi isiya ya kawaida kutoka yale yaliyoathilika kwa kiwango kidogo mpaka cha kati.  
Kufanya meno yawe meupe kwa kutumia chemikali uunguza (ixidises) rangi na kuiondoa. Chemikali zinazotumika   zina hydrogen peroxide 30%-35% na baadhi carbamide peroxide 10%. Chemikali hizi huweza kuondoa rangi zilizo sababishwa na vyakula, vinnywaji dawa za tetracycline, rangi kidogo iliyotokana na utumiaji wa madini ya magadi kwenye vyakula au kwenye maji (mild fluorosis) na mmeno yenye rangi ya yellow au grey itokanayo na umri kwenda. Inaweza kuondoa rangi itokanayo na uvutaji wa sigara na matumizi ya ugoro. Kwa wavutaji wa sigara sharti waache watumiapo chemikali hizi kwani muunganiko hydrogen peroxide na chemikali zilizopo kwenye moshi wa sigara unakisiwa kuongeza madhara ambayo tayari moshi wa sigara unasababisha kwenye mwili wa binadamu. Akina mama wanaonyosha haishauliwi pia pamoja na kwamba hakuna madhara ambayo yanajulikana mpaka sasa. 
kuboresha weupe wa meno kutumia chemikali


Kupiga meno viraka (Veneering)
Hii hufanyika kwa kuondoa sehemu ndogo ya juu ya jino kwenye enamel kama 0.5-1mm na baadae kupandika dawa yenye rangi nyeupe kulingana na mgonjwa anavyotaka mwenyewe.
Picha sikonyesha meno yaliyobadlika rangi kutokana na magadi kabla na baada ya kupigwa viraka


picha ya juu, meno yaliyoathilika na magadi kabla ya kupigwa viraka wakati ya chini ni baada ya kupigwa viraka (veneer)

Kumbuka: kuna rangi zaidi ya 26 nyeupe ambazo miongoni mwake mgonjwa anaweza kuchagua anayoitaka

1 comment:

  1. Samahani jaman. ni hospital gan naweza kupata huduma kwa arusha au moshi?

    ReplyDelete